20th April, 2018
Jamaa na marafiki wameendelea kuwasili katika chumba cha kuhifadhi maiti cha lee jijini Nairobi kuwasilisha risala za rambirambi kwa kutokana na kifo cha mbunge wa Baringo kusini Grace Kipchoim. Kipchoim ambaye alifariki mapema leo katika hospitali ya Nairobi alikokuwa akipokea matibabu kwa maradhi ya saratani ya tumbo atakumbukwa na wengi kama mbunge ambaye alichaguliwa kwa muhula wa pili na wakazi wa eneo bunge lake akiwa anaugua pasi na kufanya kampeni zozote. Baadhi ya wabunge waliofika Lee kuuona mwili wa mwenda zake wamemsifu kwa kuwa mstari wa mbele kupigania amani sawa na kukabiliana na tatizo sugu la wezi wa mifugo katika maeneo ya Samburu, Baringo na West Pokot.