20th April, 2018
Kiongozi wa NASA Raila Odinga na rais mstaafu Mwai Kibaki wamekutana mapema leo katika makazi ya kibaki mtaa wa Muthaiga hapa Nairobi. Viongozi wengine waliokuwepo kwenye mkutano huo ni gavana wa Kisumu Anyang' Nyong'o, wa Nairobi Mike Sonko, mkuu wa utumishi wa umma Joseph Kinyua, mwanawe kibaki jimmy, wakili Paul Mwangi na Nderitu Muriithi. Hata hivyo Odinga amekosa kuzungumza na wanahabari baada ya kukamilisha mkutano huo.