19th April, 2018
Wakazi wa Maralal wameitaka serikali ya kaunti kushughulikia suala la barabara kaunti hiyo kutokana na hali mbaya inayosababisha usafiri kuathirika pakubwa. Barabara ya maralal kuelekea nyahururu imebomolewa ili ujenzi kufanyika ila wenyeji wanasema imekuwa kibarua kwani mwanakandarasi hakutoa njia mbadala ya matumizi wakati wa ujenzi wa barabara hiyo. Magari sasa yamekuwa yakikwama kwenye barabara hiyo. Wanasema ni sharti hatua ichukuliwe.