19th April, 2018
Wakazi wanaoishi kandokando ya barabara ya old Namanga road sasa biashara zao zimetatizwa na maji yanayoporomoka kutoka kwenye mabomba ya maji taka. kulingana na wakazi hao, wamiliki majumba hufungulia maji taka wakati wa mvua kubwa, hali wanayosema imewasababishia uvundo huku biashara zao zikisalia kufungwa kwa kukosa wateja wanaokwepa kununua kwa maduka yao kwa sababu ya harufu mbaya.