19th April, 2018
Wazee wapatao elfu kumi huko kaunti ya Migori ambao waliratibiwa kupokea fedha za kuwafaa katika maisha ya uzee, sasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya taratibu za malipo hayo kukamilika. Wazee hao wenye umri zaidi ya miaka sabini walikusanyika katika uwanja wa michezo mjini Migori na kuhakikishiwa na mkurugenzi wa huduma za jamii kaunti hiyo Ben Makotsi, kuwa mambo yako shwari. Watakuwa wakipokea shilingi elfu nne kila mmoja kila baada ya miezi miwili.