16th April, 2018
Uhusiano mbaya kati ya baadhi ya makamishna wa IEBC na mwenyekiti Wafula Chebukati umechochea kujiuzulu kwa naibu mwenyekiti Connie Maina, Margaret Mwachanya na Paul Kurgat mapema hii leo. Watatu hao wamemlaumu Chebukati kwa matatizo ya umoja kati ya makamishna.Wiki jana, afisa mkuu mtendaji Ezra Chiloba alienda mahakamani kupinga kulazimishwa kwenda likizo ya lazima ili kutoa nafasi kwa uchunguzi wa ununuzi wa vifaa vya uchaguzi. Mahakama ilitupilia mbali ombi lake.