14th April, 2018
Maelfu ya watu wakiwemo marais kutoka pembe zote za ulimwengu wamekongamana kwenye uwanja wa michezo wa Orlando Johannesburg Afrika Kusini kumpa buriani mpiganaji dhidi ya mfumo wa apartheid mama Winnie
Madikizela Mandela. Mama Winnie Mandela aliyefariki akiwa na umri wa miaka 81 anazikwa kwenye bustani ya Fourways junction, Johannesburg.