13th April, 2018
Leo imekuwa siku njema kwa kenya, baada ya conseslus kipruto kuwaongoza wanariadha wenzake kunyakua nafasi za kwanza, pili hadi tatu, kwenye mbio za mita elfu tatu kuruka viunzi na maji.Kipruto alishinda mbio hizo na kupata medali ya dhahabu kwa kutumia dakika nane na sekunde kumi, Abraham Kibiwott akichukua nafasi ya pili kwa dakika nane na sekunde kumi na mbili, huku Amos Kirui akifunga orodha ya watatu bora