12th April, 2018
Gavana wa kaunti ya Tharaka Nithi Muthomi Njuki ametoa onyo kwa wanakandarasi kwamba huenda akalazimika kuwatupa nje baadhi yao siku za usoni. Njuki alizungumza baada ya maandamano yaliyoandaliwa na wanakandarasi hao nje ya ofisi yake wakiomba malipo ya kazi waliyofanya katika muhula uliopita. wakiandamana walilia kwamba hawakupata malipo kwa kazi nyingi walizofanya wakati huo