4th April, 2018
Wanawake na wasichana katika kaunti ya taita taveta wameanza kupokea mafunzo ya ushonaji nguo katika kituo ambacho kimeundwa katika mji wa voi. Wengi wa wanawake hao ni wajane huku wengine wakiwa wasichana waliopata mimba ya mapema. wengi wamekuwa wakihangaika kwa kukosa shughuli za kuwakimu kimaisha ndiposa hatua hiyo ya kuwapa mafunzo ya ushonaji ikachukuliwa. tayari kituo hicho kina zaidi ya wanawake arobaini na wanatarajia idadi hiyo kuongezeka hata zaidi.