3rd April, 2018
Ukosefu wa mbolea kwa wakulima North Rift sasa limekuwa kero katika eneo ambalo linategemea ukulima. Wakulima sasa wanaitaka serikali kufanikisha swala zima la kusambaza mbolea katika maduka ya jumla eneo hilo, ili wapate bidhaa hiyo muhimu kwa urahisi.