29th March, 2018
Tume ya kitaifa kuhusu haki za binadamu, chama cha wanasheria nchini na baraza la wanahabari nchini vimekashifu dhuluma dhidi ya wanahabari na wanasheria wakati wa kufurushwa nchini kwa mwanasheria Miguna Miguna. Aidha wamesema kuwa hamna sheria inayoruhusu kufutiliwa kwa uraia wa mtu alioupata kwa kuzaliwa nchini. Miguna Miguna sasa yupo Dubai kwenye himaya ya milki za kiarabu baada ya kutimuliwa jumatano usiku.