23rd March, 2018
Mwanamme wa umri wa miaka 33 alijiua kwa kujirusha kwenye timbo ya mawe iliyojaa maji. Kisa hiki kilifanyika huko Cheptiting katika kaunti ya Kericho. Walioshuhudia walisema kuwa mwenda zake alikuwa dereva wa boda boda na alikuwa ameonekana mwendo wa saa saba mchana hapo jana akaipeana pikipiki yake ioshwe kisha akaelekea kwenye timbo hiyo na kujirusha. Marehemu alipatikana na paketi ya sumu kwenye jaketi lake na kuashiria kuwa alikuwa amekusudia kujitoa uhau awali. Kamishna wa Kericho Muktar Abdi alithibitisha kisha hicho.