21st March, 2018
Siku ya kwanza ya mashindano ya gofu ya Kenya Open mchanganyiko wa wachezaji limbukeni na wazoefu ilikumbwana manyunyu ya mvua na kibaridi. Hata hivyo, kitengo hicho kiliwapa fursa wacheaji wageni kutangamana na kujifunza mengi kutoka kwa magwiji wa gofu. Mashindano hayo yanaadhimisha miaka 50 tangu yaanzishwe huku wachezaji waking'an'ania shilingi milioni 62.5 ambapo mshindi atakabidhiwa shilingi milioni10. Miongoni mwa wakenya wanaotarajiwa kuonesha ubabe wao ni Jacob Okello, Dismas Indiza, Simon Ngige, CJ Wangai na Greg Snow.