21st March, 2018
Timu ya voliboili ya wanaume ya GSU imepania kufika mkondo wa nusu fainali katika mashindano ya klabu bingwa barani, yatakayoandaliwa misri kati ya tarehe 27 mwezi huu hadi aprili 5. GSU watakuwa wanarejea tena katika michuano ya baramni baada ya kuwa nje mwaka jana katika mashindano yaliyoandaliwa nchini tunisia na walikuwa na matumaini kwamba mwaka huu huenda ukawa mwaka wao. Kocha mkuu Gideon Tarus alizindua kikosi dhabiti cha wachezaji walio na uzoefu na talanta change tayari kwa mashindano hayo.