21st March, 2018
Mamlaka ya ujenzi nchini imeanzisha mchakato wa kubomoa majumba hafifu jijini Nairobi. Shughuli hiyo ilingo'a nanga hii leo katika mtaa wa Zimmerman ambapo majumba mawili yaliyojengwa katika uwanja nyevunyevu na yasiyohitimu viwango yaliporomoshwa. Mamlaka hiyo inalenga majumba zaidi katika mitaa ya Kariobangi, Mathare na Huruma ili kuzuia maafa ya watu pale ambapo majumba yanaporomoka ghafla. Katika majumba yaliyoporomosha leo, wakaazi walikuwa wamepewa ilani ya kuhama kabla ya shughuli hiyo kuanza.