20th March, 2018
Muungano wa maaskofu kutoka Kisii kusini katika kaunti ya Kisii wametoa notisi ya siku ya saba kwa serikali kumtafuta mwenzao ambaye alipotea siku nane zilizopita. Maaskofu hao wamesema kuwa serikali haijakuwa na haraka ya kuchukulia hatua suala la kupotea kwake mhubiri Esther Bonchaberi. Esther alipotea akiwa nyumbani kwake katika kata ndogo ya bogita tarehe 11 mwezi machi kufuatia kile kinachotambulika kuwa mzozo wa ardhi. Maafisa wa usalama sasa wanasema wanachunguza kisa hicho huku wakitoa wito kwa umma kutoa ripoti yoyote kupotea kupotea kwake.