×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Moses Wetangula ang'olewa kwenye kiti chake cha kiongozi wa wachanche katika bunge la seneti

20th March, 2018

Moses Wetangula ameng'olewa kwenye kiti chake cha kiongozi wa wachanche katika bunge la seneti. Mzozo huo umekuwa ukitokota ndani ya muungano wa NASA tangu nyufa zianze kuonekana kwenye muungano huo pale maseneta wa chama cha ODM kuhisi kwamba wao ndio wanastahili kiti hicho kulingana na idadi yao ndani ya seneti. Seneta wa Siaya James Orengo anakabidhiwa kiti hicho, baada ya kubainika kwamba spika Kenneth Lusaka amedinda kuipokea barua ya afisa mkuu wa NASA Norman Magaya, iliyopinga kung'olewa kwa Wetangula. Ndio mwanzo wa kusambaratika kwa NASA? Je, upinzani umekosa makali baada ya ODM kuamua kufanya kazi na serikali ya Jubilee? Na je, Raila Odinga ana ushawishi kiasi gani  kwenye yale yaliyomfika Wetangula?

.
RELATED VIDEOS