.
15th March, 2018
Maelfu ya wakazi kutoka nchini Ethiopia wangali wanaingia Mjini Moyale kama wakimbizi kufuatia vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo katika siku za hivi karibuni.Idadi ya wakimbizi hao inaendelea kuongezeka na mashirika ya kihisani yamesema kuwa wahusika wanahitaji msaada wa dharura. Serikali ya Ethiopia ilitangaza hali ya hatari nchini humo baada ya aliyekuwa waziri mkuu Hailemarriam Desaleign kujiuzulu baada ya kushuhudiwa maandamano nchini humo.