13th March, 2018
Droo ya kombe la Chapa Dimba iliandaliwa hii leo jijini Nairobi huku timu mbali mbali zikipata kufahamu wapinzani wao kwenye kinyanganyiro hicho ambacho kitaandaliwa kutoka tarehe 22 mwezi marchi hadi tarehe 24 katika uwanja wa Bhukungu katika kaunti ya Kakamega. Washindi wa kombe hilo watapokea shillingi millioni moja kila mmoja na pia watapata fursa ya kusafiri uingereza kwa ajili ya kupokea mafunzo ya soka .