.
13th March, 2018
Rais Uhuru Kenyatta amefanya uteuzi zaidi kwenye baraza lake la mawaziri huku pia akimteua mkurugenzi wa idara ya ujasusi Noordin Mohammed Haji kuwa mkurugenzi mkuu mpya wa mashtaka ya umma. Noordin anachukua wadhifa huo uliokuwa ukishikiliwa na Keriako Tobiko, ambaye sasa ni waziri wa mazingira. Rais mpya amewateua makatibu wengine zaidi pamoja na mabalozi.