×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Mahakama kuu imetoa agizo kwa idara ya uhamiaji kufanikisha kurejeshwa nchini kwa Miguna Miguna

26th February, 2018

Mahakama kuu sasa imetoa agizo kwa idara ya uhamiaji kufanikisha kurejeshwa nchini kwa wakili anayekumbwa na utata Miguna Miguna. Kwenye uamuzi wake, Jaji Chacha Mwita ameiagiza idara hiyo pia kumruhusu Miguna kutumia paspoti yake ya Canada. Jaji Mwita amesema Miguna anahitajika kuwa nchini ili kuweza kutoa ushahidi kwenye kesi kuhusu uraia wake. Wakati huo huo, Jaji Mwita amebatilisha agizo la waziri wa usalama Fred Matiang'i kuratibisha vuguvugu la NRM kuwa kundi haramu. 

.
RELATED VIDEOS