22nd February, 2018
Mahakama imebatilisha ushindi wa Martin Wambora kama gavana wa kaunti ya Embu. Kwenye uamuzi katika mahakama kuu jaji William Musyoka ameamuru kuhesabiwa upya kwa kura zilizopigwa Agosti tarehe nane mwaka uliuopita, ambapo Lenny Kivuti alipinga matokeo ya uchaguzi huo. Wawili hao waliachana kwa tofauti ya kura mia tisa themanini na tano, kwani Wambora alizoa kura tisini na saba elfu, mia saba sitini huku aliyekuwa seneta wa Embu Lenny Kivuti akipata kura tisini na sita elfu, mia saba sabini na tano. Jaji musyoka kwenye uamuzi wake ameridhika na ushahoidi uliowasilishwa na upande wa ulalamishi kwamba vipo visa vya udanganyifu vilivyojitokeza wakati wa kura hizo. Mahakama imebaini kwamba baada ya kuamriwa kuhesabiwa upya kwa kura hizo, tofauti kati ya washidani hao wawili ilipungua ikawa finyu hata zaidi, kwa kura mia mbili tisini na tisa. Jaji ametanabahi kwamba tume ya IEBC imekiri kuwa udanganyifu ulikuwepo katika kituo cha gategi huko Mbeere kusini. Hii si mara ya kwanza kwa gavana Wambora kupoteza ushindi wake. Kwenye muhula wake wa kwanza ushindi wake uliwahi kubatilishwa kwa tuhuma za udanganyifu.