19th February, 2018
Kocha wa timu ya taifa ya kandanda Harambee Stars Paul Put amejiuzulu. Kocha huyo amejiuzulu kutokana na kile alichodai ni sababu za kibinafsi. Put aliiongoza Kenya kushinda kombe la CECAFA mwezi disemba mwaka jana . Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari kutoka kwa shirikisho la kandanda nchini ni kwamba aliyekuwa kocha wa Stars Stanley Okumbi sasa atatwaa hatamu za uongozi wa timu ya taifa kwa muda huku wakisaka kocha mkuu.