15th February, 2018
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka nchini Gor Mahia wamepanda kileleni mwa jedwali baada ya kuwacharaza Zoo FC mabao manne kwa mawili kwenye mechi iliyochezwa uwanjani Kericho. Kogalo walichukua uongozi kupitia jaques tuyisenge naye boniface omondi akaongeza la pili. Johsntone Ligare aliwasawazishia Zoo bao moja lakini kogalo wakafanikiwa kuongeza la tatu na la nne kupitia Joachim Oluoch na Samuel Onyango.