14th February, 2018
Kwenye habari nyinginezo za ajali huko Kisii, watu saba wamefariki katika barabara ya Kisii-masimba jana jioni, baada ya gari waliloabiri aina ya Toyota Probox kuwagonga dafrau wapita njia watatu na kuwaua pamoja na abiria wanne. Kwa mujibu wa OCPD wa Keroka Philip Wambugu, gari hilo lilikuwa limewabeba abiria kupita kiasi kabla ya ajali hiyo. Manusura walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya Kisii. Wito unatolewa kwa magari ya Probox kuharamishwa kutumika kama magari ya uchukuzi.