14th February, 2018
Gavana wa kaunti ya Tharaka Nithi Muthomi Njuki ameonya ya kwamba huenda wakazi wa kaunti hiyo wakajiondoa katika chama cha Jubilee iwapo Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wataendelea kuwatenga katika teuzi za serikalini. Muthomi amesema kuwa endapo rais ataendelea kuwatenga itakuwa wazi kwamba umuhimu wa kaunti hiyo katika siasa za Jubilee hauthaminiwi hivyo basi kuashiria mwanzo wa viongozi na wapiga kura kuanza mchakato wa kujiondoa kwenye chama hicho.