12th February, 2018
Mtazamaji idadi ya vijana na mchango wao katika kuendesha masuala ya taifa hili haiwezi kupuuzwa. Kusheheni kwa ukabila kunaangaziwa kuwa suala linalohitaji suluhu ya haraka ikiwa wakenya wanataka uwiano kamili. Ndiposa katika chuo kikuu cha Kisii, wanafunzi waliandaa tamasha za kila mwaka ya kuangazia tamaduni za humu nchini. Tunapozungumzia ukabila, yamaanisha tuache tamaduni zetu? Jibu ni la. Tamaduni zetu sharti ziendelee kuwepo bila kuendeleza ukabila. Ndani ya studio ninao wageni watakaozungumzia masuala hayo kwa undano ..na hawa ni Edgar Murumbu ambaye ni kiongozi wa wanafunzi chuo kikuu cha Kisii na bwana Francis Kerongo ambaye ni afisaa anayesimamia masuala ya wanafunzi katika achuo hicho, au dean of students kwa kimombo.