8th February, 2018
Mwanabondia Fatuma Zarika ametunukiwa tuzo ya mwanamichezo bora nchini wa mwezi disemba mwaka jana. Zarika aliye na umri wa miaka 34 alimbwaga catherine phiri wa zambia na kunyakua taji la wbc kitengo cha super bantamweight kwenye pigano lilofanyika mjini Nairobi tarehe mbili mwezi disemba. Ushindi huo ulikuwa wa 30 kwa mwanamasumbwi huyo, 17 ikiwa ni kwa njia ya knock out. Zarika amewapiku mchezaji chesi Joyce Nyaruayi na dereva Carl flash Tundo katika tuzo hiyo.