7th February, 2018
Serikali imebatilisha hati ya usafiri ya mwana mikakati wa muungano wa nasa David Ndii. Mkurugenzi wa uhamiaji nchini Gordon Kihalangwa kwenye barua kwa Ndii amesema kuwa ubatilisho huo umefanywa kuambatana na kipengee cha uhamiaji cha mwaka wa 2011. Kihalangwa amemuagiza Ndii kuwasilisha hati hiyo kwa idara ya uhamiaji katika jumba la nyayo kwenye muda wa siku 21 zijazo bila ya kukosa. Ndii amehusishwa pakubwa na upangaji mikakati kwenye muungano wa nasa, na hata kuhusishwa na uapisho wa hizi majuzi wa Raila Odinga, uliotajwa na serikali kuwa kinyume cha sheria.