7th February, 2018
Shirika moja lisilo la serikali limetoa msada wa kuchimba kisima cha maji kwa matumizi ya shule ya Kehancha huko kuria kaunti ya Migori. Mradi huo ni afueni kwa wanafunzi wapatao mia saba katika shule hiyo pamoja na familia zipatazo mia mbili katika eneo hilo. Mkuu wa shule hiyo Chacha Nyamohanga amewashukuru wahisani hao kwa msaada huo ambao anasema ni kichocheo kikubwa kwa viwango vya masomo.