26th January, 2018
Muungano wa upinzani, NASA, umetoa matokeo yake kuhusu uchaguzi wa tarehe nane mwaka uliopita na kudai kwamba Raila Odinga alishinda kinyangányiro hicho lakini akapokonywa ushindi. Kulingana na matokeo hayo, Raila Odinga alipata kura milioni 8.1, huku Uhuru Kenyatta akipata kura milioni 7.9. Aidha, kaimu mwenyekiti wa tume ya IEBC Connie Maina amepuzilia mbali matokeo hayo na kuyataja kama hekaya za NASA.