23rd January, 2018
Shirikisho la kandanda nchini FKF limedokeza kwamba serikali imekubali kuziba pengo la kifedha lililoachwa na wadhamini wa shiriikisho hilo ambao walijiondoa mapema mwezi huu. Rais wa shirikisho hilo Nick Mwendwa amesema kwamba shirikisho hilo pia linaweka mikakati ya kuwavutia wadhamini mbalimbali kujaza pengo hilo la shillingi milioni mia tano.