22nd January, 2018
Katibu mkuu wa muungano wa walimu nchini KNUT- Wilson Sosion pamoja na mwenyekiti wa chama cha walimu wa vyuo KUPPET- Omboko Milemba wameng'olewa kwenye sajili ya walimu ya TSC. Kwenye taarifa iliyofichuliwa hapo jana na gazeti la The Standard TSC imewaondoa kwenye sajili hiyo kwa sababu ya kuwa wanashikilia yadhifa za kisiasa. Sosion ni mbunge wa kuteuliwa wa ODM huku milemba akiwa mbunge wa emuhaya kwa tiketi ya ANC. Hata hivyo wawili hawa wamekuwa wakijitetea na kuitaja hatua hiyo ya kuwa iliyo na misukumo ya kisiasa kutoka na misimamo yao mikali.