19th January, 2018
Waziri wa afya Cleopa Mailu ameamrisha uchunguzi kuanzishwa mara moja dhidi ya madai kwamba baadhi ya akina mama wanaojifungua wamekuwa wakidhulumiwa kimapenzi na wafanyakazi wa chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali hiyo. Mwanahabari Sycilia Wakesho ambaye amekuwa akifuata taarifa hiyo anaripoti kwamba msimamizi mkuu Lily Koros ameahidi kushirikiana na idara ya upelezi kuchunguza madai hayo.