17th January, 2018
Tunaanza huko Kisii eneo bunge la bonchari ambapo ajuza mmoja wa umri wa miaka sabini na mmoja ameshambuliwa na kuuawa kufuatia kifo cha ghafla cha mjukuwe mwenye umri wa miaka kumi na miwili maxwell miruka. Wenyeji walimshuku bibi huyo kuwa amemroga mjukuwe, na ndipo wakabomoa nyumba yake iliyoezekwa kwa majani na kumteketeza moto hadi kufa. Ajuza huyo inadaiwa aliwahi kuahidi kutoa adhabu kali kwa watu waliohusika kwenye wizi wa matunda yake na hivyo basi mjukuu wake alipoaga baada ya kuugua maumivu ya kifua usiku mmoja wenyeji wakachukua sheria mikononi kwa kutumia imani za ushirikina. Polisi walichukua mabaki ya marehemu mama biyaki kemunto aliyeishi katika kijiji cha bokoma kata ya riana, na kuupeleka katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya rufaa ya kisii.