15th January, 2018
Kikosi cha Polisi al maarufu ''Chafua Chafua'' kimepokonywa taji la kitaifa la ligi ya ndondi nchini na badala yake kukabidhiwa tmu ya kdf. Hatua hii inafuatia uchunguzi uliofanywa baada ya madai ya uamuzi duni katika raundi ya mwisho ambayo ilifanyika katika uwanja wa mbuzi mwezi novemba mwaka jana ambapo timu ya polisi ilitawazwa mabingwa baada ya kuzoa alama 103. Hata hivyo, chama cha ndondi nchini kikiongozwa na mwenyekiti john kameta kimethibitisha kuwa ushindi huo haukuwa wa halali ndiposa wakaamua kuwakabidhi kdf taji hilo.