12th January, 2018
Wawakilishi wa wadi watano waliofikishwa katika mahakama ya Makueni baada ya kutiwa nguvuni na polisi hapo jana kwa kumzuia mwalimu mkuu mpya wa shule ya upili ya St. Joseph wameachiliwa kwa dhamana watano hao walitiwa nguvuni katika shule ya upili ya wasichana ya St. Joseph kibwezi kwa kumkataza mwalimu mkuu mpya rose kiragu kuanza kazi . Watano hao ni Nicholas Maitha , wa wadi ya Thange, Jades Kalunda wa Kikumbulyu south, Mirriam Musyoka na Janet Ngina. Kesi hiyo itatajwa tarehe kumi na tano mwezi ujao .