12th January, 2018
Waziri wa usalama na kaimu waziri wa elimu fred matiangi ametangaza kuwa hatajadiliana kuhusu suala la uhamisho wa waalimu wakuu. Matiangi ameongeza pia kwamba wanafunzi wa shule za upili wasioishi kwenye mabweni hawapaswi kudaiwa karo. Alizungumza kwenye warsha iliyojumuisha maafisa wa utawala na wale wa wizara ya elimu.