5th January, 2018
Wakazi wa kaunti za Embu na Kirinyagha sasa wameelezea hofu yao kuhusiana na kivukio cha rupingazi wanachosema ni hatari inawakodolea macho baada ya kusababisha vifo vya watu wengi wanaotumbukia kwenye mto.kwa mujibu wa wakazi hao kivukio hicho kilichoko kwenye barabara kuu ya embu-nairobi hakina vyuma vya reli vya kuzuiya wananchi na magari dhidi ya kuingia kwenye mto.inadaiwa kwamba zaidi ya ajali kumi na tano zimeshuhudiwa katika eneo hilo kwenye kipindi cha mwaka mmoja