29th December, 2017
Timu ya South B ilitoka nyuma na kuwalaza Beirut mabao matatu kwa mawili ili kujikatia tiketi ya fainali ya mashindano ya Koth Biro kwenye mechi iliyochezwa uwanjani Ziwani. Wakati ambapo mechi ilionekana kuisha sare ya mabao mawili kwa mawili, abraham dawo alifunga bao la ushindi kwa South B kunako dakika ya 92. Timu hiyo inasubiri mshindi wa nusu fainali ya pili kati ya fifa best na team gaa huruma itakayochezwa hapo kesho. Fainali ya mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka itakuwa tarehe 7 mwezi Januari