29th December, 2017
Wafanya biashara wa shisha wamepata afueni japo ya siku chache baada ya mahakama ya Milimani kuagiza kusikizwa kwa kesi yao kupinga marufuku ya shisha iliyotolewa na wizara ya afya hapo jana. Wafanya biashara hao kwenye ombi kwa mahakama wamedai sheria hiyo ina ubaguzi, hitilafu na ilipitishwa bila kuhusisha washikadau wote.