Fifa Best yajikatia tiketi ya tatu ya nusu fainali ya dimba la Koth Biro
28th December, 2017
Fifa Best ndiyo timu ya tatu kujikatia tiketi ya nusu fainali ya dimba la Koth Biro baada ya kuwalaza Kingstone mabao mawili kwa moja kwenye mechi ya robo fainali iliyochezwa leo uwanjani ziwani eneo la Pumwani. Musa Masika aliwapa bao la ufunguzi katika dakika ya 25 kabla ya Iregi Benson kuwafungia la pili kukiwa kumesalia dakika kumi pekee. Eugine Oduor aliwasawazishia kingstone bao moja kupitia mkwaju wa penalti lakini wakashindwa kupata la pili, Fifa wataungana na South B na Beirut katika nne bora.