6th December, 2016
Baada ya kulazwa kwenye mechi yao ya kwanza katika mashindano ya wabunge ya Afrika ya mashariki dhidi ya Uganda, hii leo timu ya Kenya ya mpira wa voliboli ilipata ushindi wa seti mbili kwa sufuri dhidi ya Uganda . Kenya ilianza mechi hiyo kwa vishindo na kupata ushindi wa seti hiyo kwa kuandikisha alama 25-14. Mashambulizi ya Kenya yalizidi kunoga katika seti ya pili na timu hiyo ikapata ushindi wa alama 25-7. Mashambulizi ya Kenya yaliongozwa na mbunge wa teso kaskazini Arthur Odera naye Isaac Sang. Hapo kesho Kenya itajitosa uwanjani dhidi ya Tanzania katika mpira wa kandanda.