28th November, 2016
Chini ya wiki mbili kabla ya mashindano ya nusu Marathon ya Afrika Mashariki kuandaliwa jijini Mombasa washindi wa makala ya mwaka jana wametunukiwa fedha zao katika shughuli iliyoandaliwa leo mjini Nairobi. Wanariadha hao ambao ni Susan Jemtai aliyeibuka mshindi katika mbio za kilomita kumi upande wa kina dada alipokea shilingi elfu 88 huku Stanley Koech na Patrick Mwenda walioshiriki mbio za kilomita 10 na 21 pia wakikabidhiwa shilingi elfu 22 na 18 mtawalia. Wanariadha wengine waliopokea pesa zao ni pamoja na James Kiplimo, Mike Kiprotich, Andrew Lesuda na Naomi Chepkoech.