22nd November, 2016
Kufuatia kukamilika kwa kandarasi ya udhamini baina ya shirikisho la raga nchini na wadhamini wao ambao ni shirika la ndege nchini KQ, Sportpesa wamechukua usukani na sasa ndio wadhamini wapya wa timu ya raga ya wachezaji saba kila upande. Udhamini huo mpya wa miaka mitano utagharimu taktribani shilingi milioni laki sita na saba na unanuiwa kuisaidia timu ya raga ya wachezaji saba kila upande kutekeleza shughuli zao kikamilifu. Vilevile udhamini huo utagawanywa kwa timu ya raga wa kina dada ya wachezaji saba kila upande na ile ya wachezaji 15 kila upande.wakati huo huo kocha wa timu ya wachezaji 7 kilaupande Innocent Simiyu ameelezeakukamilika kwa matayarisho yao ya kuelekea katika mashindano ya Dubai sevens.