1st November, 2016
Wakfu wa lotto ndio wafadhili wakuu wa mashindano ya riadha ya Baringo yatakayoandaliwa jumamosi ya tarehe 5 mwezi huu wa Novemba. Waandalizi wanahisi kwamba ndiposa michezo mbali mbali itie fora, lazima washika dau watilie maanani talanta chipuka mashinani. Mashindano haya yanafaahamika sana kwa kumzindua bingwa wa London katika riadha Mary Keitany, kama ada mashindano haya yanatarajiwa kuleta pamoja wanariadha walio na uzoefu na wale ambao wanawania kuwarithi vigogo hao. Riadha hizo za Baringo zilizinduliwa hii leo.