5th October, 2016
Bingwa wa olimpiki katika mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji Conceslus Kipruto ni miongoni mwa watakaoshiriki mbio za nyika za Ndalat Gaa mwaka huu. Zitakazoandaliwa tarehe 15 mwezi huu katika kaunti ya Nandi. Zaidi ya watu 5000 wanatarajiwa kushiriki makala hayo ya nane. Mbio hizo zimesaidia kukuza vipaji vya riadha tangu mwaka 2008 na wafadhili wana imani kuwa mwaka huu haitakuwa tofauti. Kutakuwa na vitengo vinane tofauti huku mshindi wa kitengo cha wazoefu akitia kibindoni shilingi 40000. Watakaomaliza katika nafasi ya pili hadi ishirini pia watatunukiwa.