22nd September, 2016
Baada ya kutowajibika katika makala ya olimpiki mwaka huu, kikosi cha raga cha Kenya kinarejea uwanjani nia kuu ikiwa ni mwanzo wa kujitakasa. Timu mbili za Kenya ya kwanza ikiwa ni Morans pamoja na Shujaa watajaribu kutamba katika taji la Safari 7’s na ubingwa wa afrika mtawalia wikendi hii. Na kama Moses Wakhisi anavyotuarifu, mkufunzi mkuu Benjamin Ayimba na msaidizi wake Paul Murunga wana matumaini ya kuandikisha matokeo mema.