21st September, 2016
Baada ya kungaa katika dimba la CECAFA na kumaliza katika nafasi ya pili baada ya kulazwa katika fainali 2-1 dhidi ya tanzani; kikosi cha kandanda cha kinadada wa Kenya almaarufu kama Harambee Starlets kimerejea nyumbani na kulakiwa kishujaa. Baada ya kulakiwa katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, akinadada hao pamoja na kitengo chao cha kiufundi walifululiza hadi mkahawa mmoja hapa jijini Nairobi na kuandaliwa chakula cha mchana. Starlets walistadika nchini Uganda na sasa kibarua chao ni kujiandaa ipasavyo kwa taji la kuwania ubingwa wa Afrika utakao andaliwa mwezi wa 11 kule